UHALIFU wa shambulio la kutumia
silaha,umeendelea kuibuka katika Mkoa wa Pwani,licha ya Mkuu wa Jeshi la Polisi
Nchini( IGP ),aliyeteuliwa hivi Karibuni,Simon Nyakoro Sirro,kutoa kiapo cha
kuhakikisha anaitokomeza hali hiyo,iliyowajengea hofu ya uhai wakazi wa Mkoa
huo.
Muendelezo wa matukio hayo yametokea
jana baada ya Askari Mgambo, Nurdin Kisinga (33) Mkazi wa Kijiji cha Umwe
Kaskazini Ikwiriri, wilayani Rufiji mkoani Pwani,kushambuliwa na kupigwa risasi
ya kisogoni na kusababisha kulazwa katika Hospital ya Mchukwi.
Huyu ni mgambo pili kipigwa risasi
ndani ya siku mbili baada ya Erick Mwarabu kuuawa juzi saa tisa usiku akiwa
uvunguni mwa kitanda chake.
Tukio hilo la Jumatano limetokea
katika eneo la Ngomboloni lililopo katika Kijiji cha Umwe Kaskazini ikiwa ni
takribani saa 19 tangu Mkuu wa Jeshi la Polisi(IGP), Simon Sirro kufanya mkutano
wa mazungumzo na wazee wa wilaya za Kibiti na Rufiji ili kukomesha mauaji
katika wilaya hizo.
Akielezea jinsi tukio hilo
lilivyotokea, kaka wa majeruhi aliyejitambulisha kwa jina la Kisinga Athumani
Kisinga akiwa katika Hospitali ya Mchukwi alisema ndugu yake alipigwa risasi
akiwa shambani kwake.
Alisema Nurdin alikuwa akivuna ufuta
wake shambani kwake ndipo watu ambao hawajajulikana idadi yao walimpiga risasi
moja ya kisogoni na kutokomea kusikojulikana.
Kisinga alisema Nurdin alikuwa
ameambatana na vijana wawili ambao ni watoto wake kuvuna ufuta huo.
Alisema mara baada ya kuanguka chini
wadogo zake waliomba msaada kwa kupiga yowe na ndipo mtu mmoja alifika eneo la
tukio na kumchukua kwa baiskeli hadi barabarani.
Alisema mara baada ya kufika barabarani
alifanikiwa kubebwa kwa pikipiki hadi kituo cha Polisi Ikwiriri.
Alifafanua kuwa baada ya hapo
alikimbizwa katika kitio cha Afya Ikwiriri ambapo alipatia huduma ya kwanza
kituoni hapo na baadaye alipelekwa Mchukwi kwa matibabu zaidi.
Mganga wa zamu katika hospitali hiyo
Emmanuel Humbi alisema mara baada ya kumpokea majeruhi huyo,hima walimpeleka
kwenye chumba cha X Ray kwa ajili ya uchunguzi,kabla hawajaanza kumpatia
matibabu.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI