RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, John Magufuli,amewataka watumishi wa Serikali kuwa wabunifu kwa
kuibua
vyanzo vya mapato vitakavyokuwa msaada wa kulifanya Taifa lisonge mbele
Kimaendeleo.
Wameelezwa ni vyema wakaondokana na tabia
iliyoota mizizi miongoni mwao ya kuwaza mambo
makubwa ambayo hushindwa kuyatimiza,huku wakikosa ubunifu uliotukuka unaokuwa
msaada wa kuliingizia pato Taifa.
Rais Magufuli alisema hayo wakati
akizindua Mfumo wa serikali wa ukusanyaji kodi kwa njia ya Kieletroniki,ambapo
amewaeleza kinaga ubaga baadhi ya watumishi wa Serikali wamekuwa wakiwaza mambo
makubwa ambayo wanashindwa hata kuyatimiza.
Amesema kuwa watumishi wengi wamekuwa
si wabunifu katika kuangalia vyanzo vya mapato ambavyo vinaweza kusaidia
serikali kuingiza pesa nyingi lakini wao wamekuwa wakiwaza kuongeza bei ya
pombe tu na kuacha vitu vingine ambavyo vingeweza kuongeza mapato kwa serikali
kwa njia nyingine nzuri.
Ameshangazwa kuona wanahangaika na
Machinga,katika utaratibu ambao hauna tija kwa Serikali na wahusika
wenyewe,ambao wamekuwa wakikimbizana nao mitaani.
“…. wakati tungeweza kutengeneza
vitambulisho vya wamachinga na kila kimoja tukauza labda elfu kumi, Machinga
akinunua kitambulisho hicho anatambulika na serikali na kinaeleza kuwa anapaswa
kuwa wapi, je, ni shilingi ngapi tungezipata hapo kwa idadi wa wamachinga
waliopo nchi nzima?”Anahoji.
Anaongeza kusema, “Lakini watu wetu
wao wanawaza kuongeza bei ya pombe tu, yaani tuna watu wa uchumi wengi lakini
sijui hata wanafikiria nini "
Mbali na hilo Rais Magufuli alisema
hata tabia ya watu kukwepa kulipa kodi inasababishwa na mipango mibovu akitolea
mfano kuwekwa bei juu ya kodi ya majengo jambo ambalo linafanya watu wengine
kushindwa kulipa kodi hiyo na serikali kupoteza mapato.
Anazidi kuhoji"Watu wetu hawa
hata kwenye kodi ya majengo unakuta wameweka mtu alipe milioni mbili sasa hizo
pesa wananchi wanazipata wapi?
“ Ndiyo maana wanakwepa kodi sababu
hawana pesa hizo lakini kama wangeweka labda elfu kumi, ishirini mpaka hamsini
halafu wenye maghorofa labda laki mbili ungeona kila mtu angekimbilia yeye
mwenyewe kulipa kodi, kwa nyumba zote zilizopo Tanzania tungepata shilingi
ngapi?”
Rais Magufuli anasisitiza kuwa kuweka
pesa kubwa,huku ikishindikana kuzipata inatokana na mipango mibovu,yenye
kuwakandamiza wenye vipato duni na kuwa kigezo cha kushindwa kulipa kodi hizo.
Katika hatua ya mwisho Rais Magufuli
aliyaomba makampuni ya simu nchini yawe mfano wa kuigwa na ikiwezekana yawe ya
kwanza kabisa kujiunga katika mfumo huu mpya wa ukusanyaji wa kodi kwa njia ya
kieletroniki kwani mfumo huu una manufaa kwa wawekezaji na Watanzania kwa
ujumla.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI