MDORORO
wa uzalishaji zao la Pamba,uliodumu kwa kipindi cha takribani miaka zaidi ya
Ishirini,huenda ukawa umepata muarobaini
katika Awamu hii ya Serikali ya Awamu
ya Tano,inayoongozwa na Rais John Pombe Joseph Magufuli.
Jitihada
zilizoanza kufanywa kwa kuangalia ongezeko la bei ya Pamba iliyotangazwa,kabla
kwa kuanza kwa msimu wa ununuzi wa zao hilo,imeelezwa huenda ikasababisha
ushawishi mkubwa kwa wakulima walioliasi kurejea kulima.
Mkulima
wa zao hilo,Juma Makashi,kutoka Kata ya Idahina katika Halmashauri ya Ushetu
wilayani Kahama,wakulima waliokuwa wakilima zao hilo walilikimbia na kuhamia
katika kilimo cha mazao mengine kutokana na mauzo yake kutokuwa na tija kwa
mkulima.
Mkulima
huyo alidai bei hiyo ya Shilingi 1100,ni faraja kubwa kwa wakulima wa zao
hilo,kwakuwa itawapa fursa ya pato lake kufanya shughuli zingine za
kimaendeleo,tofauti na miaka ya nyuma ambapo haikukidhi hata gharama za
uendeshaji.
Makashi
alisema kutokana na Serikali kuona umuhimu wa kuongeza bei ya zao hilo hivi
karibuni,itawezesha kuhamasisha wakulima ambao walilikimbia zao hilo kurejea
kulilima katika msimu ujao wa kilimo.
Hata
hivyo Chama cha Wakulima wa Pamba Tanzania TACOGA tawi la wilaya ya
Kahama,kupitia Kaimu Katibu Mtendaji wake,Paul Ntelya,kiliwaasa wanunuzi wa zao
hilo kufika kwa wakati kwa wakulima kufanya biashara hiyo,hatua itakayosaidia
kutoharibika kwa zao hilo.
“…mkulima
akinunuliwa zao lake na kupata malipo yake kwa wakati,itamjengea hamasa ya
kufanya maandalizi kwa msimu unaofuata,kwa kuweka malengo ya kukuza kilimo
chake,pia kuwa sababu ya kuwavutia wengine kuamua kulima pamba.”Alisema Ntelya.
Aidha
Tacoga iliwaasa wakulima kuwa waaminifu katika zoezi zima la uuzaji zao hilo la
Pamba,kwa kuwataka kutotumia mifuko ya sandarusi kufungia zao,kwakuwa imekuwa
chanzo cha kulichafua na badala yake watumie nguo za khanga,vitenge ama mifuko
ya pamba,kama vifungashio.
Ntelya
aliwatoa hofu wakulima wa zao hilo kuwa katika msimu huu hakutokuwepo
udanganyifu katika mizani,kutokana na Bodi ya pamba,kuandaa ukaguzi
utakaoambatana na Mhakama inayotembea,ambapo Mnunuzi atayebainika kumuibia
Mkulima atahukumiwa papo hapo.
Hata
hivyo aliwaomba wakulima wasiwe waoga kutoa taarifa katika vyombo vinavyohusika
pindi wakiona wanafanyiwa dhuruma katika mauzo yao.
Msimu
wa zao la Pamba unatarajiwa kufunguliwa Juni 5,mwaka huu katika Kijiji cha Mwabusalu
wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu,huku kukiwa na ongezeko la Shilingi Mia Moja katika
kila kilo moja ya pamba itakayouzwa.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI