Wananchi wakiwa nyumbani kwa marehemu Jacob Paul leo mchana |
Mwenyekiti wa Chama Cha Waendesha Pikipiki maarufu bodaboda manispaa ya
Shinyanga Jacob Paul (36) amejiua kwa kujinyonga kwa kutumia waya wa
simu chumbani kwake katika mtaa wa Mwinamila kata ya Ngokolo katika
manispaa ya Shinyanga.
Tukio hilo limetokea leo Jumamosi June 10,2017 mchana.
Tukio hili limetokea siku tano tu baada ya kutokea vurugu kati ya
waendesha bodaboda na polisi baada ya mwendesha bodaboda mwenzao
kufariki baada ya kukamatwa na askari wa usalama barabarani
Jacob Paul enzi za uhai wake
Chanzo:-Malunde 1 blog