NI Simanzi na huzuni kubwa umeupata familia ya soka nchini,hususani Klabu ya Dar Young African,kuondokewa na shabiki
wake,mpenzi wake na Mhamasishaji mwenye vibweka vya aina yake,Ally Mohammed,kufariki dunia.
wake,mpenzi wake na Mhamasishaji mwenye vibweka vya aina yake,Ally Mohammed,kufariki dunia.
Shabiki huyo amekumbwa na umauti huo katika ajali ya gari eneo la kijiji cha Chipogoro wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma.
Kifo cha shabiki huyo kimepokewa kwa majonzi na masikitiko makubwa na Uongozi wa klabu ya Yanga SC kufuatia taarifa ya kifo cha aliyekuwa shabiki wao mkubwa
aliyefahamika kwa jina la Ally Yanga.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma Lazaro Mambosasa amethibitisha kifo cha aliyekuwa shabiki maarufu wa klabu ya soka ya Yanga Ally Yanga kilichotokea leo katika ajali ya gari aina ya Rav4.
Katika taarifa iliyotolewa na klabu hiyo
imesema kifo cha shabiki huyo kimeacha pengo kubwa kwa nafasi yake
ambayo ilipelekea kujipatia umaarufu mkubwa pamoja na kuwa balozi mzuri
kama mwanachama wa timu hiyo.
Enzi za uhai wake Ally Yanga atakumbukwa
kutokana na mbwembwe zake alizokuwa akizionesha za kujipaka masizi ya
mkaa usoni pindi klabu ya Yanga ikiwa uwanjani.
Ally
Yanga ambaye pia ni mkereketwa wa Mwenge wa Uhuru alikutwa na mauti
akiwa katika gari la kampuni ya Faidika ambalo lilikuwa kwenye shughuli
zake za promosheni na SIO KWAMBA alikuwa kwenye msafara wa Mwenge kama
inavyoenezwa.
Lakini
tangu baada ya uchaguzi Mkuu Novemba 2015, Ally Yanga ameadimika
viwanja vya soka kutokana na kujikita zaidi kwenye shughuli za Chama cha
Mapinduzi CCM.