Friday, June 9, 2017

BAJETI YA 2017/18..WAMACHINGA,MAMA LISHE KUSAJILIWA NA KUPEWA VITAMBULISHO..!!! *ADA YA MWAKA YA LESENI YA MAGARI YAFUTWA…! *YAFUTA USHURU WA HUDUMA KATIKA MA-GUEST! *MADINI KUKAGULIWA KABLA YA KUSAFIRISHWA…!

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



SERIKALI sasa kuwatambua wafanyabiashara wadogo wadogo wasio rasmi wakiwamo mama lishe na baba lishe,machinga kwa kuahidi kuwapa
vitambulisho maalumu vitavyosaidia kuwatambua rasmi.


Aidha  haitaruhusu usafirishaji wa madini moja kwa moja kutoka mgodini na kupelekwa nje ya nchi.Huku ikitangaza kufuta rasmi kwa ada ya mwaka ya leseni ya magari.


Hayo yalielezwa jana Alhamisi na Waziri wa Fedha na Mipango, Phillip Mpango wakati akiwasilisha hotuba ya bajeti kwa mwaka 2017/18.  Ambapo alibainisha kwamba vitambulisho hivyo vitawasaidia kutengewa maeneo maalumu ya kufanyia biashara.

Akiwasilisha mapendekezo ya bajeti kuu kwa mwaka wa fedha 2017/18,ambayo ilikuwa ikishangiliwa kwa vifijo na nderemo na wengi wa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mpango alisema hatua hiyo inalenga kuwasaidia wafanyabiashara hao ili kukuza mitaji yao.


Sambamba na hilo Serikali imetangaza kufuta ushuru wa huduma  kwenye nyumba za kulala wageni.



Pamoja na ushuru huo, pia Serikali imefuta ushuru wa mabango yanayoelekeza mahali zinapopatikana huduma za kijamii kama vile shule na hospitali.


Kadhalika alisema Serikali kwa dhati imeamua kufuta tozo la malipo ya leseni wa gari,ambao ulikuwa ukilipwa kila mwaka.

Alisema  uamuzi huo umechukuliwa ili ada hiyo ilipwe mara moja pale gari linaposajiliwa na baada ya hapo iendelee kulipwa katika ushuru wa bidhaa  katika mafuta ya petroli na dizeli.


Pamoja na hayo, Waziri Mpango ameshusha ushuru  kwa mvinyo  unaotengenezwa kwa zabibu zinazozalishwa  ndani kutoka Shilingi 2O2  kwa lita hadi Shilingi 200 kwa lita.

Hata hivyo alisema ushuru wa bia zinazotengenezwa kwa nafaka za ndani umepanda kutoka Shilingi 429 hadi 450 kwa lita.

 Wakati huo, ushuru wa  bia zisizo na kilevi na vinywaji vya kuongeza nguvu kutoka Shilingi 534 hadi Shilingi 564 kwa lita.

Aidha alisema Serikali imesitisha utaratibu uliokuwa ukifanywa na Wawekezaji katika shughuli za madini nchini za kusafirisha bidhaa hiyo moja kwa moja kutoka viwanja vyao vya Migodi,badala yake kutakuwa na viwanja maalumu vya kimataifa katika bandari, migodini na madini hayo yatathibitishwa na kupewa kibali kabla ya kusafirishwa nje.

“Kibali hicho kitatozwa ada ya asilimia moja ya thamani ya madini hayo,” amesema.

Amesema Serikali itatangaza rasmi tarehe rasmi ya kuanza  kwa ada hiyo.




KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI