Tuesday, May 30, 2017

WANAFUNZI SEKONDARI KAHAMA,WAGEUZA VIVULI VYA MITI KUWA BWALO.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO




MAPEMA Januari,Mwaka huu,bweni katika Shule ya Sekondari Mwendakulima,liliteketea kwa moto na kusababisha
wanafunzi kuanza kuishi katika mazingira ya tabu.

Katika ajali hiyo ya moto,ambayo haikusababisha madhara ya kifo ama jeraha kwa mwanafunzi yeyote,imekuwa sababu ya wanafunzi hao kupata chakula wakiwa nje kufuatia bwalo lililokuwa la chakula,kutumika kwa ajili ya kulala wanafunzi.

Wanafunzi katika shule hiyo yenye Kidato cha kwanza hadi cha sita,wamejikuta wakilazimika kuketi katika vivuli vya miti,muda unapowadia wa chakula,kitendo kinachodaiwa kupunguza ari ya kusoma kwa wanafunzi hao.

Hali hiyo ilielezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kahama,Anderson Msumba,katika uzinduzi wa ujenzi wa jengo jipya la bweni ulioambatana na msaada wa vitabu 1312 vya masomo ya Sayansi kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne vyenye thamani ya Shilingi Milioni 24,vilivyotolewa na Mgodi wa Buzwagi.


Msumba alibainisha tangu kuungua kwa bweni hilo,Januari mwaka huu,kumelazimisha vijana wanaosoma katika shule hiyo,kupata chakula wakiwa wameketi chini ya miti,kufuatia uongozi wa shule hiyo kuligeuza bwalo kuwa chumba cha malazi,kitendo ambacho wana imani kinashusha morari ya vijana kusoma.

Alisema kwamba kabla ya tukio la moto,waliwasilisha maombi katika Mgodi wa Buzwagi usaidie kujenga bweni lingine kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi kufuatia shule hiyo kuwa na kidato cha kwanza hadi cha sita,ombi ambalo lilikubaliwa na uongozi wa Mgodi.

“..lakini kabla ombi hilo kutekelezeka,bweni lililopo likaungua na kusababisha wanafunzi waishi katika mazingira magumu,huku mgodi ukiwa kimya katika kutekeleza ahadi yake,nilikata tamaa,sasa nafarijika kuona umedhamiria kukamilisha ahadi yake.”Alisema Msumba.

Kwa upande wake,Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi unaomilikiwa na Kampuni ya ACACIA,Stewart Hamilton,alisema watahakikisha ahadi zote walizoahidi zinatekelezeka,kuanzia zile za sekta ya elimu hadi sekta ya afya.

Alifafanua katika mradi waliahidi wa ujenzi wa bweni,wamepanga kutumia Shilingi Milioni 214,na kwmba jengo hilo litakapo kamilika litasaidia kurejesha hali ya kawaida shuleni hapo kwa matumizi ya bwalo kutumika kama ilivyokusudiwa.

Nae Makamu Mkuu wa Shule hiyo,Sonda Kenda,alisema msaada wa vitabu waliopokea sambamba na kuanza kwa mradi wa ujenzi wa jengo la Bweni,wameutarajia kwa kipindi kirefu na utajenga hamasa kubwa kwa wanafunzi kuhakikisha wanafanya vyema katika masomo yao kwakuwa yatakuwa yamewajengea mazingira mazurin ya kupata elimu.



KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI