Tuesday, May 30, 2017

ACACIA BUZWAGI YAIKUMBUKA MAGEREZA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

IDARA ya Magereza Nchini ni moja ya Taasisi muhimu nchini,kutokana na kuwajibika kulinda katika maisha ya kila siku;Watuhumiwa na Wafungwa,wanaojumuika nao
katika maisha ya kila siku kwa mujibu wa sheria,huku askari wake wakikabiliwa na changamoto ya kuishi katika Mazingira Duni.
Changamoto hizo zimeuvuta Mgodi wa Dhahabu wa Buzwagi,unaomilikiwa na Kampuni ya Uchimbaji madini ya ACACIA,kutumia Jumla ya Shilingi Milioni 12.8,kujaribu kupunguza changamoto ya makazi inayoikabili Idara ya Magereza wilayani Kahama,ambayo askari wake wanaishi familia nne katika nyumba moja.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Gereza wilaya ya Kahama,SSP Isani Mjimbi,alisema Idara hiyo ina changamoto kubwa ya makazi kutokana na kuwa na nyumba kumi na sita huku baadhi yake zikiwa duni,hali iliyowafanya kuomba msaada katika Mgodi huo.


Katika makabidhiano ya vifaa hivyo,Meneja wa Mgodi wa Dhahabu Stewart Hamilton,alisema wametoa vifaa hivyo ikiwa ni jukumu lao la kusaidia huduma za jamii katika wilaya ya Kahama,baada ya kuombwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya,kusaidia idara hiyo.


Alisema msaada huo ni katika jitihada za kuunga mkono,Idara ya Magereza wilaya ya Kahama za kujenga Maboma kwa lengo la kupunguza upungufu  wa nyumba za makazi kwa askari ambao wamekuwa wakiishi katika makazi duni,huku wakilazimika kuchangia nyumba moja zaidi ya familia nne.


Hamilton alivitaja vifaa vilivyotolewa kwa ajili ya kukamilisha boma moja lenye uwezo wa kubeba familia nne,ni mifuko ya saruji 51,bati 96,misumari kilo 29,milango 12,trip 10 za michanga,Trip nne za kokoto na trip sita za mawe.


Akizungumza wakati wa kupokea Misaada hiyo,Mkuu wa Gereza la Kahama, SSP Isani Mjimbi,alisema idara hiyo yenye jumla ya askari 80 inakabiliwa na upungufu wa nyumba zaidi ya  kumi,huku zilizopo 16 zikidaiwa kuwa ni chakavu kutokana na kujengwa mwaka 1957.


SSP Mjimbi alisema kutokana na nyumba zilizopo kuwa pungufu na nyingine zikiwa duni hali imewafanya askari kuishi katika mazingira  magumu yanayowalazimisha askari kugawana chumba kimoja kimoja kwa kila familia.


Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kahama,Fadhili Nkurlu aliziomba taasisi na makampuni mbalimbali wilayani Kahama,kujitokeza kutatua changamoto zinayoikabili Idara ya Magereza,kutokana na umuhimu wake katika Jamii.


Nkurlu alisema Idara hiyo pamoja na kukabiliwa na matatizo mbalimbali imekuwa ikionesha jitihada za kufyatua tofari na kujenga maboma,hivyo jamii sambamba na  mashirika pia kampuni zinapaswa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na idara hiyo katika kujinasua na makazi duni.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI