Sunday, January 29, 2017

MJUKUU WA KAPUYA ATUNGA KITABU CHA SHULE YA MSINGI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



WAKATI Januari 15,mwaka huu,Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) ikitangaza wanafunzi 67,547 wa darasa la Nne nchini,kurudia darasa hilo,kutokana na mtihani uliopita kupata alama zenye ufaulu usioridhisha.

Huku wanafunzi waliofanya mitihani hiyo,wakishindwa zaidi katika masomo ya Hisabati na Kiingereza,Mjukuu wa aliyekuwa Waziri katika wizara kadhaa za Serikali ya Awamu ya Tatu na ile ya
Awamu ya Nne;Professa Juma Kapuya,ametunga kitabu cha ziada kwa somo la Kiingereza.

Mjukuu huyo wa Professa Kapuya;Farid Hamamad,ametunga kitabu hicho kujaribu kupunguza changamoto inayoikabili Serikali ya uwepo wa vitabu vya ziada katika shule za msingi nchini,hususani katika somo la kiingereza ili kuleta chachu ya wanafunzi kufanya vyema katika mitihani yao ya mwisho.

Hamamad anasema anatambua umuhimu wa sekta ya elimu kwa maslahi ya Taifa,pia changamoto iliyopo ya uhaba wa vitabu vya ziada katika shule za msingi ambavyo uwepo wake kwa wingi huku vikitumika ipasavyo ni siri ya ufaulu mzuri wa wanafunzi.

Anasema maendeleo ya kiuchumi ya Taifa lolote duniani ni sekta ya elimu,na kwakuwa kiu yake kubwa kuona Tanzania inamiliki uchumi imara,ambao chachu yake itakuwa ni wasomi ndio maana kapata hamasa ya kuandika kitabu cha somo hilo ambalo mara nyingi huwa kikwazo cha ufaulu mzuri kwa wanafunzi.

“Tunaupungufu wa vitabu vya ziada nchini,hasa katika shule za msingi,hususani kwa somo la Kiingereza,ndio maana hata ufaulu wake kwa watoto waliofanya mtihani wa darasa la nne,mwaka jana ni asilimia 12.51,nimeumia sana kwa ufaulu huo kwa Taifa ambalo lina mkakati wa kukuza uchumi wake kwa kuanzisha viwanda,ndio maana nimeona nisaidie kwenye hilo,”alisema Hamamad.

Anabainisha kwamba kitabu hicho cha ziada,kina maswali na majibu kwa wanafunzi,ambayo ni mazoezi yatakayokuwa msaada kwao wa kufanya vyema katika mitihani ya Kiingereza kwa darasa la nne na ile ya kuhitimu elimu ya msingi,pindi wakikitumia vyema kwa kufanya mazoezi ya kutosha.

Katika mitihani ya darasa la nne iliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana,wanafunzi 1,054,191 walisajiliwa,lakini waliofanya mtihani walikuwa 1,017,776 na miongoni mwao asilimia 6.64 wakipata alama za daraja E,lenye ufaulu usiorodhisha na hivyo kulazimika kurudishwa mwaka huu kusoma darasa la nne tena.

Wanafunzi walifanya vyema katika somo la Stadi za Kazi,Haiba na Michezo kwa kufaulu kwa asilimia 94.67 na kuanguka zaidi katika somo la Kiingereza.  

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI

1 comments:

Write comments
Unknown
AUTHOR
January 29, 2017 at 8:14 PM delete

Analosema Hamamad ni la kweli kabisa, tunachangamoto nyingi sana katika elimu Tanzania, Nakupa pongezi kwa kujitokeza kusaidia wanafunzi mashuleni, waweze kuelewa na kufahamu lunga ambayo inatumika ulimwengu mzima katika kila sekta ya Maisha, hususan Uchumi. Kila mwenye kipaji chake akikutumia kwa lengo la kukuza elimu, na kusaidia watanzania wenzake, Tanzania itakua Nchi Bora na Imara katika bara la Africa na Ulimwengu kiujumla

Reply
avatar