Tuesday, October 11, 2016

SAMSUNG GALAXY NOTE 7 NI HATARI,ZAPIGWA STOP!

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



ONYO limetolewa la jamii duniani kuepuka kuendelea kutumia simu ya kiganjani aina ya Samsung Galaxy Note 7,kwa madai kuwa zimekuwa zikiripuka hivyo kuweza kusababisha madhara kwa mtumiaji.

Tamko la zuio la matumizi ya simu hiyo,limetolewa na kampuni ya Kikorea,inayotengeneza simu za Samsung,kwa kuwataka watumiaji wake kutupa toleo la ‘Galaxy Note 7’, kutokana na kuwepo kwa ripoti za matukio mengi ya watumiaji wa simu za Samsung kulipukiwa na simu hizo wakati wa kuchaji.

Kampuni ya Samsung imetoa tamko rasmi kupitia tovuti yake ikiwataka watumiaji wa simu hizo toleo la ‘Galaxy Note 7’ duniani kote kuchukua tahadhari na kuacha kabisa kuzitumia  wakati ikiendelea na uchunguzi zaidi.

Taarifa hiyo imeeleza kwamba inafanya kazi kazi na Mamlaka husika kufanya uchunguzi kuhusu kuwepo kwa ripoti za matukio yanayohusu Galaxy Note7. Kwa sabababu Kampuni hiyo suala la usalama kwa wateja kwao ni kipaumbele.

Hivyo taarifa hiyo ya Samsung imewataka wauzaji wote wa simu hizo duniani kuacha mara moja kuuza Galaxy Note 7,hadi hapo uchunguzi wao utakapokamilika na kujiridhisha kuwa hazina madhara.

Majaribio ya betri ya simu ya Samsung, Galaxy Note 7 yaliyofanywa katika maabara moja nchini Singapore yalipelekea simu hiyo kulipuka moto.

Hivi karibuni, hata hapa Tanzania, kumekuwa na ripoti za matukio ya wananchi wengi kudai kuwa wameripukiwa na simu za Sumsung walipokuwa wanachaji. 

Pia, kulikuwa na taarifa ambazo hazikuthitishwa na Mamlaka kuhusu watu kulipukiwa na simu hizo walipozipokea wakati zikiwa kwenye chaji.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI