Tuesday, June 13, 2017

SHINYANGA KUKUZA UCHUMI WA MKOA KWA KILIMO CHA ALIZETI.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



WAKULIMA Mkoani Shinyanga,wameshauriwa kulima zao la Alizeti,kutokana na kuwa na fursa kubwa ya kukuza uchumi wa mkoa kufuatia
uwepo wa Mwekezaji anayezalisha mafuta huku akikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa malighafi ya bidhaa hiyo.

Sambamba na uwepo wa Mwekezaji,ambaye ufanisi wake umekuwa mdogo kutokana na ukosefu wa malighafi ya kutosha,pia wakulima wanaweza kumudu kumiliki mitambo yenye gharama nafuu ya kukamulia mafuta,hivyo kujiongezea kipato.

Mwenyekiti wa Kanda ya Ziwa wa Umoja wa Wazalishaji wa Mbegu za Mafuta ( TEHOSA),Paul Ntelya, alitoa ushauri huo,huku akisisitiza zao hilo linaweza kuwa mkombozi wa Mkoa kumudu kuanzisha viwanda vidogovidogo vya utengenezaji wa mafuta kwa wajasiriamali.

Ntelya alisema pindi wakulima wakilima zao hilo ana imani uchumi wao utakuwa kwa kasi,kutokana na zao hilo mafuta yake kupendeka kwa kiwango kikubwa,ndani na nje ya nchi,huku ukamuaji wake ukitegemea viwanda vidogo vidogo vinavyoweza kumilikiwa hata na Mkulima Mmoja.

“ Zao hilo limekuza kwa kasi uchumi wa mkoa wa Singida,kutokana na bidhaa yake kuhitajika kwa wingi,na utengenezaji wake hauhitaji mitambo mikubwa,sasa mkoa wa Shinyanga una ardhi bora zaidi,ni imani yangu utafanya vyema zaidi ya Singida,”alisema Ntelya.

Aidha alisema pindi Wakulima wakililima zao hilo kama la biashara itasaidia kwa kiwango kikubwa kwa Mwekezaji wa Kiwanda cha Mafuta ya Alizeti cha Mkoani Shinyanga ambacho uzalishaji wake unakabiliwa na changamoto ya malighafi za kutosha.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga,Zainab Telack,katika ziara yake ya kikazi wilayani Kahama,aliwaasa Madiwani na Wabunge,kuwahamasisha wakulima kuzalisha malighafi ambazo zitaongeza thamani ya kilimo chao na kuuza katika viwanda vya wawekezaji waliopo Mkoani Shinyanga.

Alisema Wawekezaji waliopo mkoani Shinyanga,wanakabiliwa na changamoto za malighafi ili kumudu kuendesha shughuli zao walizowekeza,hivyo ni jukumu la wakazi wa Mkoa wa Shinyanga,kunufaika kwa kukuza uchumi wao na Taifa kwa ujumla kwa kuzalisha malighafi zitakazokuwa na tija kwa Mwekezaji.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI