UMOJA wa Wazee wilayani
Kahama(UWAKA),umeibuka na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania,John Pombe Joseph Magufuli,juu ya hatua alizochukua kuhusiana na
kufichua ufisadi uliokuwa ukifanyika katika mchanga wa dhahabu ( Makinikia
),baada
ya kuona Halmashauri zao zinachelewa kutoa pongezi.
Aidha Uwaka umezishangaa Halmashauri za Msalala na Mji zilizo wilayani
Kahama,kwa kushindwa kujitokeza kumpongeza Rais Magufuli,kuwafichua wanaotorosha
mchanga wa madini(Makinikia),ilhali Halmashauri hizo ndio waathirika wakubwa.
Wakiongea kwa masikitiko
makubwa,katika kikao chao maalumu,Wazee hao wa Uwaka,walidai Halmashauri hizo
mbili ndio waathirika wakubwa,hivyo walitaraji Mabaraza ya madiwani
yangeitishwa kwa vikao vya dharura,ili kuunga
mkono juhudi za Rais na kumpongeza kwa kuwafichua mafisadi wa Makinikia.
Katibu wa Uwaka,Paul Ntelya,alisema alichokifanya Rais hakikutarajiwa na kimemgusa kila Mtanzania mzalendo mpenda Maendeleo kinastahili kupongezwa ili kumuunga mkono kwa jitihada za kuwafichua wezi wa mali za nchi.
Katibu wa Uwaka,Paul Ntelya,alisema alichokifanya Rais hakikutarajiwa na kimemgusa kila Mtanzania mzalendo mpenda Maendeleo kinastahili kupongezwa ili kumuunga mkono kwa jitihada za kuwafichua wezi wa mali za nchi.
“ Tulitegemea Halmashauri zetu hizi
mbili,kupitia Mabaraza yetu,zingeliketi pamoja na kutoa tamko,maana kwa upande
Bulyanhulu ilipo Halmashauri ya Msalala,imeathirika tangu mwaka 1998,huku
Halmashauri ya Mji ulipo Mgodi wa Buzwagi wenyewe tangu 2001,huku zikiwa na
madai yao lakini zimekaa kimya,”alisema Ntelya.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
Uwaka,Bathlomew Kayoka,alisema Halmashauri hizo zilistahili kuitisha mabaraza
ya dharura yenye vimelea vya uzalendo,kutoa pongezi kwa niaba ya wananchi wa
maeneo hayo ambao hawanufaiki na huduma za jamii kutoka migodi hiyo kulingana na thamani ya
mali wanayovuna.
“ Sisi wazee hili limetugusa na
kutusisimua sana,kwani limetoa matumaini ya maendeleo chanya kwa jamii yetu,ama
hakika tuna Rais mzalendo,hivyo kwa niaba ya wana Kahama,tumedhamiria kufikisha
pongezi zetu hizo kupitia kwa Mkuu wa wilaya ya Kahama,”alisema Kayoka.
Nae Mzee Deogratias Mulumba,alisema
pamoja na kutoa pongezi hizo,wana Kahama hawana budi kushinikiza Kampuni ya
Acacia kuwajengea vyuo vitatu vyenye hadhi,ambapo alianisha vyuo hivyo kuwa ni
budi kiwepo cha VETA,Afya na Elimu,hatua itakayosaidia wakazi wa eneo hilo
kuona wamenufaika japo kidogo kuwepo kwa Mwekezaji huyo.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Halmashauri
ya Mji wa Kahama,Abeli Shija,akiongea kwa njia ya simu na gazeti hili,alidai
waliita baadhi ya vyombo vya habari(Hili halikuwa katika Mwaliko)na kutoa tamko
la kumpongeza Rais Magufuli,siku hiyo hiyo alipokabidhiwa taarifa ya pili ya
Uchunguzi juu ya Makinikia.
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI