Thursday, June 15, 2017

BODABODA WAWASHUSHIA KISAGO MATAPELI WA USALAMA BARABARANI

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO

VIJANA wanaofanya biashara ya kusafirisha abiria kwa kutumia pikipiki almaarufu;Bodaboda,wameshindwa kudhibiti hasira zao na kuchukua sheria mkononi baada ya kubaini wanafanyiwa Utapeli,na watu waliokuwa wakifanya shughuli za askari wa usalama barabarani kinyume cha sheria huku wakijipatia fedha.
Madereva hao wa Bodaboda hizo,hawakuwa na simile baada ya kubaini mchezo huo mchafu uliikokuwa ukifanya na Watu wawili waliokuwa wakidai kuwa ni Askari wa Usalama barabarani,ndipo walipowavamia na kuwajeruhi vibaya baada ya kuwababatiza wakiendeleza hila ya kutekeleza jukumu la ukamataji wa pikipiki zisizo na leseni.

Tukio hilo limetokea katika kijiji cha Katunguru kata ya Katunguru wilayani Sengerema wakati watu hao ambao hawakuweza kujulikana majina yao walijeruhiwa sehemu mbalimbali za miili yao, baada ya kuanza kukamata pikipiki pasipo kuwa na vitambulisho vya kazi pamoja na kutovaa sare za Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani.
Wameongeza kuwa baada ya kuwashambulia watu hao kwa kuwadhania kuwa wezi wa pikipiki, walikili kuwa wao sio maaskari wa Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani wala hawahusiani na jeshi la polis lakini walikuwa wakitumiwa na Jeshi la Polisi kituo cha katunguru kukamata pikipiki.
Madereva hao waliliomba Jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani  kuhakikisha shughuli za ukamataji wa pikipiki zina simamiwa na maaskari wenye weledi wa kazi hiyo ilikuepuka mataperi wa pikipiki ambao wamekuwa wakitumia nafasi ya Jeshi la Polisi kuiba pikipiki hususani kwa madereva pikipiki.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi alipohojiwa alisema Ofisi yake haija pokea taarifa za tukio hilo na kuahidi kufuatilia tukio hilo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI