Wednesday, April 26, 2017

VISIWA UKEREWE KUPATA UMEME WA JUA

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO


ZAIDI ya wananchi 40,600 katika visiwa 10 vilivyopo wilayani Ukerewe,wanaokabiliwa na  changamoto ya ukosefu wa
aidi ya wananchi 40,600 katika visiwa 10 vilivyopo wilayani Ukerewe,wanaokabiliwa na  changamoto ya ukosefu wa
umeme kufuatia miundombinu kutokuwa rafiki, wanatarajia kuondokana na adha hiyo.

 Serikali kupitia Mwekezaji;Rex Energy  imejipanga kutoa huduma hiyo ya umeme,wa nishati ya jua chini ya uangalizi wa  Rural Energy Agency (REA) ikiwa ni kuhakikisha wanajamii wanaishi katika mazingira salama,anaandika Tunu Herman,aliyekuwa wilayani Ukerewe.

Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Rex Energy,Mhandisi Francis Kibhisa,amewahakikishia wakazi wa visiwa hivyo kumi,kuondokana na adha hiyo kwakuwa wako tayari kuihudumia jamii.

 Akizungumza katika hafla fupi ya uzinduzi wa mpango huo ulioambatana na utiaji saini mkataba wa ujenzi wa miundombinu ya nishati ya umeme wa jua katika visiwa hivyo,baina ya Serikali kupitia Halmashauri ya wilaya ya Ukerewe na Mwekezaji,kwa kuwataka wananchi kuwa na imani,kwakuwa wamedhamiria kuiondoa changamoto hiyo.

Amesema,“Wananchi waishio katika visiwa mbalimbali hapa nchini wamekuwa wakipata shida ya kuishi gizani kufuatia kukosa umeme,huku serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli, ambayo inaitaka Tanzania iwe ya Viwanda.”

“….. sisi  Rex Energy kama wazalenzo tumeamua kuwekeza katika sekta ya nishati ya umeme wa jua ambao utakuwa ni rahisi kuwafikia wanachi wengi walio katika maaeneo korofi ikiwa na kumudu gharama za utumiaji ili kuweza kukuza uchumi kwa wananchi ikiwa na kujishugulisha na shughuli mbalimbali za kimaendeleo,”alisema Kibhisa.

Ujenzi huo wa mradi katika visiwa 10 umegawanyika katika awamu mbili ambapo visiwa vya Ghana,Bwiro,Kamasi,Burubi ambavyo tayari viko katika awamu ya kwanza na viko  katika hatua ya kukamilika na gharama yake ni Bilioni 6.4.

Amefafanua kuwa visiwa vya  Kweru kuu,Kweru Mto,Izinga,Zeru,Bushengele na Sizu vitakamilika katika awamu ya pili na gharama yake ni Bilioni 14.6.

Aidha Kibhisa alisema wakati wakiendelea na shughuli hiyo watajikita katika masuala makuu matatu amabayo yako ndani ya jamii ikiwa ni kuboresha mazingira ya shule,ujenzi wa Zahanati na Visima vya maji salama katika visiwa hivyo ,ili kuweza kwenda sambamba na maendeleo ya sehemu husika.

Mkazi wa kisiwa cha Ghana, Tatu Nyerere,akizungumza kwa niaba ya wananchi wanaoishi katika visiwa hivyo alisema, wanakabiliwa na changamoto za ukosefu wa vituo vya Afya vinavyopelekea adha kubwa kwa wamama wajawazito kujifunglia njiani ikiwa na kupoteza maisha.
“Tunaishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kutuletea wawekezaji wazalendo ambao wanafahamu wananchi wamaeneo mengi wanahitaji nini, leo tumempata Rex Enegy amabaye ametuletea umeme,atatujengea vituo vya afya kuboresha shule na visima vya maji salama,”

“……kwakeli tunamshukuru maana tulikuwa tunaishi katika maisha hatarishi ya kukumbwa na vifo vinavyoweza kuepukika,magonjwa ya milipuko tunaamini hata suala la ulinzi na usalama litakuwa lipo katika visiwa husika,”alisema Tatu.

Naye mkurugenzi wa halmashauri hiyo,Frank Bahati, alisema wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto ya miundombinu kutokana na Jiogorafia ya eneo hilo kuwa mbalimbali,hali inayochangia kuchelewa kwa maendeleo   hivyo kuishukuru Rex Energy kwa kuamua kutatua changamoto zilizopo ndani ya jamii ya Ukerewe.



KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI