Monday, April 24, 2017

MATUKIO YA MOTO NI CHANGAMOTO KAHAMA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



AFISA wa Jeshi la Zimamoto na Uokaji  Wilaya ya Kahama,Mkaguzi Msaidizi Frank Elophazy,amesema kikosi chake kinakabiliwa na
changamoto za mawasiliano na miundo mbinu isiyo rafiki ya uokozi pindi matukio ya moto yanapotokea.

Wilaya ya Kahama,imeelezwa kukua kasi,ambapo ina Halmashauri tatu za;Msalala na Ushetu sambamba na Mji ambapo ndipo yalipo Makao Makuu ya Jeshi hilo kwa wilaya ya Kahama,huku kukiwa na gari moja kwa ajili ya uzimaji moto,kwa halmashauri zote tatu,anaandika Lutufyo Kanyenye.

Elophazy alikiri kutokana na kukua kwa Mji wa Kahama,kumesababisha kuwepo kwa  matukio mengi ya moto tofauti za miaka ya nyuma,ambapo mengine yamesababishwa na miundo mbinu ya awali ya utandikaji nyaya za umeme majumbani kuchoka.

Amefafanua miundo mbinu hiyo ya awali,inashindwa kukabiliana na  nishati ya umeme,yenye nguvu kutoka Mgodini Buzwagi,tofauti na ule wa awali,na kubainisha tatizo hilo limeishapata ufumbuzi baada ya kuketi na watu wa Tanesco,ambao wanahamasisha wateja wao kubadili na kuweka miundo mbinu imara.


Mkaguzi msaidizi huyo,anasema licha  ya umbali katika Halmashauri mbili za Ushetu na Msalala,pindi yatokeapo matukio ya moto.Kwa upande wa Mji,hukumbana na changamoto ya ujenzi holela wa nyumba za makazi na biashara,zilizo kikwazo cha kukabili kwa wakati tukio la moto.

Amezidi kubainisha kwamba ukubwa wa eneo wanalostahili kutoa huduma hiyo,limesababisha kutokidhi uzimaji moto kwa wakati kutokana na gari wanalomiliki kutokuwa na ujazo mkubwa wa maji,hivyo kulazimika kuomba kuongezewa lingine lenye ujazo zaidi.

Anasema,“Kamishina alipofanya ziara mkoani kwetu,tuliwasilisha maombi ya kuongezewa gari kubwa,tumepatiwa gari lenye uwezo mkubwa wa kubeba kiasi cha lita 18,000 tofauti la lile la awali ambalo lililokuwa likibeba lita 4000,ama lile la Buzwagi tuliliomba kuongezewa nguvu ambalo nalo lilikuwa na ujazo wa lita 6000.”

“….lakini changamoto iliyopo gari hilo linahitaji matengenezo makubwa yanayogharimu Shilingi Milioni  14.5,ambazo tunalazimika kuzipata  kwa michango ya wadau,kibali tumepatiwa kutoka ofisi nya mkuu wa wilaya,tunaomba wafanyabiashara na jamii nzima ituunge mkono kufanikisha  matengenezo,”alisema Elophazy.

Wilaya ya Kahama kwa mwaka jana ilikuwa na matukio ya moto 30 huku ya uokozi yakiwa manne,kwa kipindi Januari hadi April 18,kulikuwa na matukio ya moto 19  na uokozi 12,jambo lilisababisha kuombwa kwa gari hilo ili kuongezea nguvu yaliyopo.

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI