Monday, February 13, 2017

WATANO WATUMBULIWA HALMASHAURI YA MSALALA.

BOFYA HAPA CHINI KUONA MAAJABU YA LEO



BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Msalala Wilaya ya Kahama,Mkoani Shinyanga limewatimua  kazi watumishi wake wa watano wa idara mbalimbali,kutokana na makosa tofauti tofauti,akiwemo muuguzi  aliyempiga makofi mgonjwa.

Maamuzi hayo yamefikiwa kutokana na Baraza hilo,kujigeuza kamati ya nidhamu,kuketi na kupitia taarifa za uchunguzi za watumishi mbalimbali baada ya kubaini mapungufu ya kinidhamu,kisha kuchukua maaamuzi hayo kwa mujibu wa kanuni za utumishi wa umma za mwaka 2003.

Akitangaza maamuzi hayo yaliyobarikiwa na madiwani hao,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala,Mibako Mabubu,alisema katika kikao cha kamati ya nidhamu ya madiwani kilipokea mashauri nane na kujadiliwa,ambapo walibaini upungufu huo wa nidhamu,na kuchukua maamuzi hayo sambamba na kumvua madaraka mtumishi mmoja na kutoa onyo kwa wengine watatu.

Alisema maamuzi hayo yametokana baada ya kubaini ukosefu wa nidhamu kazini sambamba na utoro kwa watumishi hivyo kuwataka watumishi wabadilike nakuongeza kuwa kama mfanyakzi ambae hatakwenda na kasi ya awamu ya tano ni bora akaacha kazi mapema, kabla baraza halijamjadili na kumchukulia hatua za kisheria.

Mwenyekiti huyo aliwataja waliofukuzwa kazi kuwa ni Joyce Makewa,ambaye ni Ofisa Muuguzi msaidizi wa daraja la pili,aliyechukuliwa maamuzi hayo baada kumpiga makofi mgonjwa huku akiwa ameitumikia halmashauri hiyo kwa kipindi cha miezi 13.

Mabubu alimtaja mwingine kuwa  ni  Elikana Silasi Masota, ambae alikuwa na cheo cha Afisa uvuvi Msaadizi,ambae alikaa katika kituo chake cha kazi mwa muda wa miezi 40 nakubainika kuwa na utoro wa siku 70 hali ambayo kamati iliazia mtumishi huyo kufukuzwa kazi.

Aliwataja watumishi wengine waliofukuzwa kuwa ni Edward Lotta ambae ni afisa wa wanyama pori daraja la pili ambae alikaa katika kituo chake cha kazi kwa muda wa miezi 13 huku akibainika kuwa na utoro wa siku 75,pia Maximilian Kasongo alikuwa mtumishi wa idara ya afya aliyekaa katika kituo chake cha kazi kwa muda wa miaka 8 huku akibainika kuwa na utoro wa siku 115.

Mtumishi mwingine aliyetimuliwa ni Wencesilaus Charles, Mhandishi wa ujenzi daraja la pili aliyekaa katika kituo chake cha kazi miezi 14 alikufukwa kazi kwa kosa la utoro wa siku150.

Aidha alimtaja, Ester Nduguru ambae alikuwa mhudumu wa afya aliyekaa katika kituo chake cha kazi kwa miezi 20 alibainika kuwa na utoro wa siku tatu ambao sii zaidi ya siku tano kisheria hakukutwa na hatia na kamati imeridhia kurudishwa kwenye orodha ya malipo ya mishahara.

Hata hivyo aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Ujenzi katika Halmashauri;Pharles Ngeleja,amevuliwa wadhifa baada ya kubainika kuidhinisha mitambo ya ujenzi kwenda nje ya mkoa  bila idhini ya Mkurugenzi huku akiwa ameitumikia miezi 15,kitendo ambacho ni kutumia madaraka yake vibaya lakini ataendelea na kazi yake ya uhandisi.

Mtumishi wa mwisho alisema kuwa ni Syvester Machiya ambae alikuwa ni fundi msanifu ujenzi mkuu aliyekaa kazini ndani ya miaka 4 na alikuwa akitumia bila idhini ya mamlaka husika mali ya mwajiri wake hivyo kamati ilianzia kumtoa hatiani mtumishi huyo.

Mabubu alimuonya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Simon Berege,kusimamia mamlaka yake vema kwa  kuchukua hatua kali kwa kila mtumishi atakaekwenda kinyume na taaraibu za kazi,vinginevyo asipochukua hatua za kisheria kwa watumishi hao, Baraza litaanza na mkurugenzi kisha kwenda kwa watumishi wengine.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala,Simon Berege,anatoa onyo kwa watumishi kuzingatia nidhamu kazini na kuzingatia uwajibikaji na hata sita kumchukulia hatua yeyote atakayekiuka misingi yake ya kazi.

Anasema “Serikali ya awamu ya tano inazingatia uwajibikaji,nami nitamuwajibisha kwa hatua kali za kitumishi yeyote atakayekiuka misingi yake ya kazi sintongoja Baraza ambalo mchakato wake ni mrefu kufikia maamuzi haya.”




  

KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI