WANAFUNZI wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Lushelo Kata ya Kinamapula;Alfred Amos na Marco Robart wakionyesha umahiri mkubwa wa kucheza muziki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Ukimwi. |
Vijana.
Hali
hiyo ilibainishwa katika maadhimisho ya kumbukumbu za Ukimwi Duniani
zilizofanyika kiwilaya kata ya Kinamapula katika Halmashauri ya wilaya ya
Ushetu na Diwani wa Kata ya Mpunze,Benedicto Mabuga ambapo alisema takwimu
zinaonyesha vijana wengi kuathirika na maradhi hayo.
DIWANI wa Kata ya Mpunze Benedicto Bundala akikabidhi zawadi kwa ajili ya watoto wanaoishi katika mazingira magumu baada ya kufiwa na wazazi wao. |
Diwani
Mabuga alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Kahama,Benson Mpesya alisema
takwimu zinaonyesha vijana kati ya miaka 15 hadi 49 idadi kubwa wameambukizwa
virusi vya Ukimwi hali inayoonyesha kuwepo kwa mwingiliano mbaya wa kimapenzi
baina yao na watu wazima.
Hata
hivyo Mabuga amesema pamoja na changamoto hiyo halmashauri yake ya Ushetu
ambayo ni moja ya halmashauri zingine mbili za mji na Msalala zilizopo wilayani
Kahama imeweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na janga hilo
WASANII wa Kahama Medical Culture Troupe walitoa burudani katika maadhimisho hayo. |
Kwa
upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ushetu Anna Ngongi alisema Jumla
ya watu 5200 katika Halmashauri hiyo wanaishi na virusi vya ukimwi na tayari wamejiunga
na huduma ya kliniki ya tiba na mafunzo huku 2800 kati yao wameanza
kutumia dawa ya kupunguza makali ya ugonjwa wa ukimwi
Katika
taarifa ya Halmashauri hiyo juu ya maambukizi ya Ukimwi, Ngongi alisema idadi
hiyo ni kubwa kwa kuwa ni sawa na asilimia 5 tofauti ya alama moja ya takwimu
za kitaifa za asilimia 5.1 hali ambayo jamii inatakiwa kushilikiana kuweka
nguvu za pamoja kupambana na janga hilo
KUONA VIDEO MPYA BOFYA HAPA CHINI